Mara nyingi watu wanapoongelea kupamba nyumba wanazingatia zaidi sebule na sehemu zingine na kulisahau kabisa jiko.
Jikoni pia linafaa kupendeza ili kumpa mpishi hamu ya kupika na hata
kumpa mlaji hamu ya kula Chakula kama kikipikwa katika mazingira safi
na mazuri.Kwa upande mwingine hata wewe mpishi unapata nguvu ya kuwepo
jikoni endapo utaweka jiko lako katika mazingira mazuri.
Wengi hawapambi na kutengeneza jiko kwa madai ya kuwa na gharama
kubwa ya maboresho hayo ili hali wageni huwa awafiki jikoni lahasha ,
Ukweli ni kwamba hiki ni kisingizio kisichofaa hata kidogo kwani kupamba
au kutengeneza jiko zuri si lazima utumie gharama kubwa hata kuweka
mpangilio mzuri wa jiko ni urembo tosha.
Kuna mambo madogo unayoweza kufanya ili kupendezesha jiko lako na kulipa mvuto kwa kufanya haya:
1.Mpangilio wa vitu: Ili jiko livutie ni lazima liwe
na mpangilio mzuri na wenye nafasi, Kupanga huku kunahusisha meza za
jikoni,vyombo kabatini,ndoo,majiko,friji na kila kikaacho jikoni.
Jitahidi vyombo vyote vikae ndani ya kabati la vyombo na kama kabati ni
dogo na vyombo ni vingi basi tunza ndani ya Boksi au mabeseni makubwa
ili mradi tu visisambae jikoni.
2.Matumizi ya rangi zinazo ng’ara: Rangi
zinazong’ara hupendezesha sana jiko,ni vyema kununua vitu vyenye rangi
za kung’ara ili kung’arisha zaidi jiko.Rangi hizo ni kama
Kijani,njano,nyekundu,bluu,nyeupe ,orenji na zingine.
3.Urembo wa aina mbalimbali: Ni vyema kuwa mbunifu
na kutumia urembo wa aina mbalimbali kupendezesha jiko.Unaweza tumia
vyungu vya aina mbalimbali na rangi mbalimbali kwa kuvipanga juu ya
kabati au sehemu nyingine yoyote.
4.Vyombo vizuri: Vyombo vizuri hulipa jiko
mvuto,nunua vyombo vyenye maumbo na rangi mbalimbali.mfano badala ya
kununua sahani za duara kila mara unaweza nunua sahani za pembe nne au
zenye umbo la yai.
6.Ondoa vitu usivyotumia: Ni vyema ukaondoa jikoni
kitu chochote usichotumia,kwani vinachukua nafasi na kujaza jiko bila
sababu.watu wengi hupenda kutunza vitu wasivyotumia kama majiko
mabovu,vyombo vibovu na kadhalika
Tabia hii ni mwanzo wa uchafu jikoni,na uwepo wa mende na panya.Pia
hufanya mtu asinunue vitu vipya kwa kujipa moyo kua anavyo,wakati ukweli
ni kwamba alivyonavyo ni vibovu na havifai.
No comments:
Post a Comment