TTCL

EQUITY

Thursday, December 3, 2015

Ukaguzi makontena tisa waendelea Dar

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) inaendelea Uchunguzi na ukaguzi kwenye makontena hayo tisa yaliyokamatwa juzi, ambapo moja tayari limebainika kuwa na vifaa vya ujenzi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo, alisema Mamlaka hiyo ilianza kufungua makontena hayo juzi usiku kwa baadhi ya makontena.

Alisema makontena hayo ambayo ni mali ya Heritage Empire Company Ltd yenye namba ya mlipakodi (Tin) 116536501, bado wanaendelea kuyakagua kwa kutoa vifaa vyote vilivyomo ndani yake.

"Tuliyafungua juzi jioni na wamiliki wa makontena hayo walikuwepo, moja ya makontena hayo lilikuwa na vifaa vya ujenzi hivyo kwa kuwa hatutaki kuwaamini moja kwa moja kwamba kuna vifaa vya ujenzi pekee, ndiyo sababu hivi sasa tunaendelea na kazi ya kupakua mzigo wote ili kujiridhisha," alisema Kayombo.
Aliongeza kuwa watakapokamilisha uhakiki wa kodi waliyolipa ndipo itatolewa taarifa kama ipo sawa au hapana.

Kontena hizo zilishikiliwa na Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Jumatatu usiku baada ya wasamaria wema kutoa taarifa, hivyo kuleta viashiria kwamba huenda ni mzigo wa wakwepa kodi.

Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka kwa Ofisa Elimu huyo wa TRA, makontena hayo yalikuwa yanapelekwa APZD katika eneo la Ubungo badala yakeyakapelekwaBarabara ya Bagamoyo ambapo yalikamatwa maeneo ya Mbezi tanki bovu baada ya kutiliwa shaka. 

No comments:

Post a Comment