TTCL

EQUITY

Friday, November 22, 2013

Taarifa maalum kutoka TANESCO kuhusu tatizo la mgawo wa umeme na Ukomo wake..


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema, machungu ya mgawo wa umeme unaoendelea sasa yatapungua  kuanzia leo baada ya kukamilika kwa asilimia 85 ya matengenezo ya Kisima cha Gesi cha Songosongo mkoani Lindi.
  
 
Matengenezo ya kisima hicho yaliyoanza Novemba 16 mwaka huu, yamesababisha kushuka kwa uzalishaji wa umeme na hivyo kuathiri shughuli mbalimbali za uzalishaji  na huduma za jamii. 
Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud alisema, hatua hiyo inatokana na kuzimwa kwa mitambo ya Kampuni ya Pan African iliyoko Songosongo ili kuruhusu  matengenezo.
Alisema mgawo huo ulipaswa kuwa wa saa mbili lakini imeshindikana kwa sababu nishati hiyo inakosekana kwa zaidi ya saa 12 kila siku.
 
Badra alisema maeneo yanayoendelea kuathirika ni Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Tanga, Arusha na Zanzibar.
Hali kadhalika mikoa mingine kadhaa.
Kaimu Mkurugenzi wa Tanesco, Felchesmi Mramba alisema kupungua kwa mgawo huo kunatokana na matengenezo ya visima vya gesi.
 
Alisema shirika linatarajia kupokea  asilimia 80 ya gesi kuanzia jana jioni, tayari kwa uzalishaji wa umeme na kwamba hatua hiyo itaongeza upatikanaji wa nishati katika maeneo yaliyoathirika.
Mgawo utapungua kutokana na kiasi cha asiliami 80 ya gesi kitakachoanza kuingia leo (jana),” alisema.

Visima vya Songosongo siyo mali ya Tanesco,  Tanesco inanunua gesi kutoka kwa Songosongo ambao  wakiwa na matengenezo wanatupa taarifa tu,” alisema Mramba.

No comments:

Post a Comment