WASANII wa
muziki wa kizazi kipya Bongo, Hamad Ally ‘Madee’ na Juma Saidi ‘Chege’
wikiend hii watazindua video (vichupa) za nyimbo zao mpya ndani ya
Ukumbi wa Club Bilicanas, jijini Dar es Salaam.
Zuwena Mohamed ‘Shilole’.
Akizungumza
na gazeti hili juzikati, ‘Rais wa Manzese’ Madee alisema katika
shughuli hiyo watasindikizwa na mkali wa kibao cha Nakomaa na Jiji,
Zuwena Mohamed ‘Shilole’.
Hamad Ally ‘Madee.
“Mimi
nitatoa video ya wimbo wangu mpya wa Tema Mate Tuwachape ambao
nimeufanya na Studio ya Ogopa Djs wa Kenya na Chegge yeye atakuwa na
video ya kibao chake cha Ubinadamu ambao pia ameufanyia Ogopa,” alisema
Madee.
Alisema
siku hiyo (Jumapili hii) kutakuwa na red carpet ambapo mashabiki
watapiga picha na mastaa wao huku Chegge pia akizindua mtandao wake (Web
site).
No comments:
Post a Comment